Kilele cha mkutano wa dharura wa Jumuia ya Ushrikiano wa
Kiislamu (OIC) kimefikia tamati yake mjini Makka kwa kusisitiza juu ya kulinda
umoja wa Waislamu na kusimama imara dhidi ya “fitna” katika nchi za Kiislamu.
Pamoja na hayo, mkutano huo ulikuwa na maazimio yafuatayo:
1.
Mkutano mkuu umetaka kusimamishwa haraka
matumizi ya nguvu nchini siria pamoja na kulipeleka mbele ya umoja wa Mataifa
suala la Waislamu wachache wa BURMA (MYANMAR) wanaonyanyasika na kukandamizwa.
2.
Wamelipokea na kulikubali pendekezo la mfalme
Abdullah ibn Abdulaziz wa Saudi Arabia la kuanzisha kituo maalumu kwa ajili ya
mazungumzo na maelewano baina ya Madhehebu za Kiislamu, kitakachokuwa na makao
makuu mjini Riayadh, Saudia.
3.
Viongozi wa
nchi za Jumuia hiyo yenye wanachama 57 ambao wanawakilisha zaidi ya watu
bilioni 1.5 duniani, wamekubaliana juu
ya “umuhimu na ulazima wa kulinda umoja wa nchi ya Syria na ardhi zake na
kusimamisha mara moja matumizi yote ya nguvu pamoja na kusitisha uanachama wa
Syria katika Jumuia ya Ushirikiano wa Kiislamu.”
4.
“Azimio la Makkah” limetaka “baadhi yetu
kujitenga dhidi ya kutumia misimamo ya kimakundi na kimadhehebu katika
kutumikia siasa na malengo yake badala ya kutumia siasa kwa ajili ya kuitumikia
dini.”
5.
Tamko la azimio hilo limesisitiza “kusimama safu
moja pamoja na jamii za Kiislamu zinazonyanyaswa na kuonewa mbele ya macho na
masikio ya walimwengu wote na kukabiliana
na uadui wa kutisha unaofanywa dhidi ya wananchi wasiokuwa na msaada,
wanaouawa na kuteswa.”
6.
Vilevile azimio hilo limesisitiza juu ya kusonga
mbele katika “mapambano dhidi ya ugaidi na fikra potofu zinazosababisha suala
hilo, kuulinda umma dhidi ya hilo janga na kutoyaruhusu makundi yanayochafua
historia ya umma huu pamoja na kitabu chake na sunna za Mtume Wake.”
7.
“Kusimama safu moja katika kupambana na fitna
ambazo zimeanza kupenya ndani ya kiwiliwili
cha Uislamu kwa misingi ya ubaguzi, madhehebu na makundi. Suala hilo
litawezekana kwa kuheshimu utukufu na uhuru wetu na kutoingilia masuala ya
ndani kwa kigezo cha nchi moja kuisimamia nchi nyingine na kwa kisingizio cha
aina yoyote ile.”
8.
Vile vile azimio limetoa jukumu zito kwa vyombo
vya habari katika “kuondosha fitna na kuimarisha misingi na malengo ya
ushirikiano na mshikamano wa Kiislamu.”
9.
Pamoja na hayo, viongozi hao wa nchi za Kiislamu
walitilia mkazo juu ya “umuhimu wa kadhia ya Palestina kwa kuizingatia kadhia
hiyo kuwa ni mhimili wa umma wa Kiislamu na kukomesha ukaliaji wa mabavu wa
Israel kwenye ardhi za Waarabu na Palestina tangu mwaka 1967 ikiwemo msikiti
mtukufu wa Quds. Waliubebesha utawala vamizi wa Israel lawama ya kukwama kwa
mazungumzo ya pande husika.
10.
Kwa upande mwingine, viongozi hao wa nchi za
Kiislamu wameazimia kulipeleka suala la Waislamu wa Burma mbele ya Baraza Kuu
la Umoja wa Mataifa, huku wakikosoa vikali matumizi ya nguvu yaliyofanywa na
watawala dhidi ya Waislamu hao.
Katika azimio la mwisho la Jumuia ya
Ushirikiano wa Kiislamu, viongozi hao walielezea “masikitiko yao makubwa kwa
utawala wa Myanmar (Burma) kutumia nguvu dhidi yao na kuwanyima haki ya uraia.”
Katibu Mkuu wa Jumuia ya Ushirikiano wa
Kiislamu, Ekmeliddin Ihsanoglu katika
mkutano wake na waandaishi wa habari baada ya kikao cha mwisho cha Mkutano huo,
alisisitiza kuwa viongozi wote wa Jumuia, katika mazungumzo yao, walijikita
sana katika kadhia ya Waislamu wa Myanmar (Burma), jambo linaloisisitizia Jumuia ya Kimataifa na
Serikali ya Burma kwamba “zaidi ya Waislamu bilioni moja na nusu wamesimama
nyuma ya Waislamu wa Burma.”
Mkutano huo ulikosoa vikali kile
ulichokiita “uhalifu wa kibinaadamu” unaofanywa na Serikali ya Myanmar dhidi ya
Waslamu wa chache wa nchi hiyo.
“Azimio la Makka” lilisisitiza kuwa “siasa
za manyanyaso na matumizi ya nguvu zinazofanywa na serikali ya Myanmar dhidi ya
raia wake Waislamu ni uhalifu dhidi ya ubinaadamu na ni jambo linalotakiwa
kukosolewa na kupingwa vikali na mataifa yote ya ulimwengu wa Kiislamu kwa
namna ya kipekee na mataifa ya ulimwengu mzima kwa ujumla.”
Viongozi hao wa nchi za Kiislamu wameitaka
“Serikali ya Myanmar kuacha haraka vitendo hivyo na kuwapa Warohingya haki zao
kama raia katika nchi ya Myanmar.”
Mkutano huo ulioitishwa na mfalme wa Saudi Arabia,
ulihudhuriwa na marais wa nchi wapatao 40.
No comments:
Post a Comment