Friday, March 23, 2012

Tangazo la Mashindano ya Kimataifa

Al Azhar Al Sharif
Mkusaanyiko wa Tafitit za Kiislamu
Idara kuu ya Mambo ya Baraza la Mkusanyiko na Kamati zake.

(Uwezo wa Kuran Tukufu na Sunnah za Mtume S.A.W. zilizotakasika juu ya mwenendo wa Elimu ya Mazingira)

 Kamati ya Uwezo wa elimu ya Kuran na Sunnah za Mtume Mtakasifu ya Azhar Asharif kwa kushirikiana na Bank Faisal ya Kiislamu tawi la Egypt, inawatangazia kuwa itaandaa Mashindano ya Kimataifa juu ya (“Uwezo wa Kuran Tukufu na Sunnah za Mtume S.A.W zilizotakasika juu ya mwenendo wa Elimu ya Mazingira

Kwa masharti yafuatayo:-
  • Mosi: - Utafiti uandikwe kati ya lugha mbili: - Kiarabu au Kiingereza.
  • Pili: - Utafiti utakaoletwa kwa mshindano usiwe kwa kiwango cha kielimu au umepewa zawadi nyingine.
  • Tatu: - Utafiti uweke wazi juu ya uhakika wa kielimu ambao umetanguliwa na Kuran pamoja na Sunnah Takasifu.
  • Nne: - Utafiti uandikwe kwa Kompyuta na usipungue kurasa mia moja na zisizidi kurasa mia mbili, pamoja na Ufupisho ulio nje ya Utafiti usiopungua kurasa kumi na usiozidi kurasa ishirini pamoja na CD inayohusu utafiti huo.
  • Tano:- Utafiti pamoja na Ufupisho wake upelekwe na taarifa binafsi ya mashirika (C.V.) kwa nakala tatu kwenye Kamati ya Uwezo wa Kuran Tukufu na Sunnah za Mtume – Mkusanyiko wa Tafiti za Kiislamu Nasr City mpaka mwisho wa mwezi Mei 2012 na mpelekaji wa utafiti huo atapewa risiti iliyogongwa.
  • Sita: - Baada ya kupitiwa kwa tafiti na wahusika washindanaji wataitwa wenyewe kwa wale waliopendekezwa kufuzu na kupewa zawadi za mali kwa kiwango cha:- 

Paundi Elfu Hamsini na Tano za Kimisri (55,000/=) kwa washindani ishirini na tatu (23) kama ifuatavyo:- Paundi 15,000 elfu kumi na tano kwa mshindi wa kwanza.  Paundi 10,000 elfu kumi kwa mshindi wa pili. Paundi 5,000 elfu tano kwa ,mshindi wa tatu.

Na zawadi tano (5) za kutia moyo zitatolewa kwa watu watano ikiwa kila mmoja atapata Paundi Elfu mbili (2,000/=)

Na zawadi kumi na tano (15) nyingine za kutia moyo zitatolewa kwa watu watano ikiwa kila mmoja atapata Paundi Elfu moja (1,000/=)

  • Saba: - Watapewa taarifa washiriki wa shindano sehemu na siku ya sherehe ya kuzawadia washindi.
  • Nane: - Tafiti iliyoshinda haitarejeshwa kwa mwenyewe, kwani tafiti hiyo itahifadhiwa kwenye ofisi za Kamati maalum kwenye jingo la ofisi za Azhar Asharif, ama kwa tafiti zisizoshinda zitarudishwa kwa wenyewe kwa kipindi cha miezi miwili tokea tarehe ya sherehe ya kugawa zawadi.
  • Tisa: - Kwa mwenye kutaka kujifanyia waqfu achapishe na kusambaza yale atakayopata toka kwemye tafiti ya mshindi, kwa gharama ya waqfu bila idhini na haki toka kwa mshindi.
  • Kumi:-Tangazo hili linahusu Vyuo vVkuu vyote na Vituo vya eEimu pamoja na Magazeti na wasambazaji – kama habari isiyo na malipo – kwa Magazeti na Majarida mbalimbali.

Mwenyezi Mungu ndiye Mwezeshaji wa kila jambo.

Kamati ya uwezo wa Elimu ya Kuran Tukufu na Sunnah za Mtume zilizotakaswa Mkusanyiko wa Tafiti za Kiislamu

No comments:

Post a Comment