Friday, March 23, 2012

Uvimbe Katika Mlango Wa Kizazi (Cervicitis Polyps)

Uvimbe huota ndani ya kizazi (leiomyoma au Fibroid - vinyama ambavyo vipo kama uvimbe laini).

Chanzo Ni Nini?
Uvimbe (fibroid au Uterine Myoma) husababishwa na kuwepo kiwango kikubwa cha mafuta katika maeneo ya kizazi na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha Estrogen hormones.Vinyama hivi vinapokuwa katika mlango wa kizazi mwanamke huhisi kama kuna kitu ukeni kimechomoza na anapojisafisha hukigusa na anaposhiriki tendo la ndoa huhisi kuna kitu kinaguswa au kusukumwa ndani ukeni. Kinyama hicho kinapoguswa mara kwa mara husababisha mwanamke kutokwa na damu ukeni pia husababisha damu ya hedhi kutoka kiasi kidogokidogo ikiambatana na maumivu ya tumbo chini ya kitovu, kutokwa na majimaji yenye rangi ya brown ukeni yakiambatana na harufu mbaya. Tatizo hili likikaa muda mrefu husababisha mlango wa uke (cervix) hivyo hata upatikanaji wa mimba huwa na matatizo, damu ya hedhi kutoka kwa shida ikiandamana na maumivu makali ya tumbo chini ya kitovu na kutokwa na mabonge meusi ya damu'D.U.B'.

Vipimo
Ultrasound,Cervical Xray na vingine kuangalia ukeni kama ambavyo Dkt. ataona vinafaa.

Tiba na Ushauri
Baada ya uchunguzi wa kina tiba hutolewa kutokana na ukubwa au udogo wa tatizo. Ukiona dalili mathalan kutokwa na damu wakati wa tendo wahi kwa Dkt.

Makala Hii Imeandaliwa Na Dokta Abdulazizi Maliki 

Simu:
+255714 909563
+255763 986499

No comments:

Post a Comment